Home » » BARIADI KUTUMIA BILIONI 4.9/- KUJENGA STENDI

BARIADI KUTUMIA BILIONI 4.9/- KUJENGA STENDI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Imeandikwa na Shushu Joel, Bariadi
HALMASHAURI ya mji wa Bariadi, Simiyu imesaini mkataba wa Sh bilioni 4.9 na kampuni ya JV Kings & Helem Contractors ya Dar es Salaam kujenga stendi ya kisasa ya mabasi Somanda na kilomita 1.5 za barabara ya lami.
Akizungumza kabla ya kusaini mkataba huo, Mkurugenzi wa Halmashauri ya mji wa Bariadi Melkizedeck Humbe, alisema fedha za mradi huo zimetolewa kwa mkopo na Benki ya Dunia.
Alisema mradi huo utajumuisha ujenzi wa nyumba na ujenzi wa barabara hiyo kutoka Bariadi Sekondari hadi Nyamhimbi na barabara ya Ikulu kwenda ofisi ya Mkuu wa Mkoa. Alisema mkataba huo utatekelezwa ndani ya mwaka mmoja na akawataka wakandarasi hao kuzingatia mikataba kuhusu suala la mazingira.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya mji wa Bariadi, Robart Lweyo alisema ujenzi huo utaharakisha maendeleo kwani miundombinu ikikamilika halmashauri hiyo itapata ushuru wa mabasi.
Lweyo alimtaka mkandarasi huyo kuzingatia muda wa mkataba huo akisema baadhi ya wakandarasi wanafanya miradi mingi mwisho wake inawashinda kukamilisha kwa wakati. Mhandisi wa JV Kings & Helem Contractors, Happy Lebe alisema watajitahidi kutekeleza mradi huo kwa haraka ili ikiwezekana wakamilishe kabla ya mkataba huo kuisha.
CHANZO HABARI LEO

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Simiyu Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa