Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mhandisi Baraka Felix kutoka Kampuni ya EAU Consult akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe.Angelina Mabula(Mb)(kulia) alipotembelea eneo la hekta 13 katika Kijiji cha Kalago, Kata ya Lamadi, Wilayani Busega lililokuwa linamilikiwa na Mwekezaji Hermati Pateli kinyume cha sheria, ambaye amefutiwa hati na Serikali.
Mhandisi Baraka Felix kutoka Kampuni ya EAU Consult akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe.Angelina Mabula(Mb)(kulia) alipotembelea kuona Ujenzi wa Ofisi ya Mamlaka ya Maji Lamadi itakayosimamia mradi wa maji wa Lamadi unaojengwa katika eneo lililokuwa linamilikiwa na Mwekezaji Hermati Pateli kinyume cha sheria, ambaye amefutiwa hati na Serikali .
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe.Angelina Mabula(Mb) (kushoto) akipokea maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega, Anderson Njiginya wakati alipotembelea eneo la hekta 13 katika Kijiji cha Kalago, Kata ya Lamadi, Wilayani Busega lililokuwa linamilikiwa na Mwekezaji Hermati Pateli kinyume cha sheria, ambaye amefutiwa hati na Serikali.
Na Stella Kalinga, Simiyu
Naibu
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Angelina
Mabula(Mb), ameziagiza Halmashauri nchini, kuyatambua na kuyatolea
taarifa maeneo yanayohodhiwa na watu bila kuendelezwa na yale ambayo
hayakupatikana kihalali ili Wizara iweze kuchukua hatua stahiki.
Naibu
Waziri huyo ameyasema hayo alipotembelea eneo la hekta 13 katika Kijiji
cha Kalago, Kata ya Lamadi, Wilayani Busega lililokuwa linamilikiwa na
Mwekezaji Hermati Pateli kinyume cha sheria, ambaye amefutiwa hati na
Serikali, kisha Halmashauri ya Busega Mkoani Simiyu kuanza ujenzi wa
mradi wa maji katika eneo hilo utakaonufaisha vijiji vinne vya kata ya
Lamadi.
Mhe.Mabula
amesema Halmashauri zinapaswa kutambua maeneo yasiyoendelezwa na
yanayomilikiwa kinyume cha sheria na kuwasilisha taarifa katika Wizara
ya Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi ili yaweze kuyarejesha kwa
wananchi na kupangiwa matumizi mengine yenye manufaa zaidi kwa jamii.
0 comments:
Post a Comment